Friday, February 1, 2019

Hivi Ndivyo Zari Alivyowaumbua Tanasha na Shilole

Hivi Ndivyo Zari Alivyowaumbua Tanasha na Shilole

Mchumba wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Tanasha Donna Oketch ameendelea kutengeneza vichwa vya habari Bongo, Amani linaye.

Safari hii Tanasha amekuwa gumzo kufuatia gauni alilovaa kwenye pati ya uzinduzi wa pafyumu na taasisi ya Msemaji wa Simba, Haji Sunday Manara, usiku wa kuamkia Jumatatu iliyopita ambalo limeibua mapya.



Gauni hilo la rangi ya bluu linashabihiana kila kitu na lile lililowahi kumuumbua mwanamuziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ au Shishi Baby miezi kadhaa iliyopita.

Lakini mzazi mwenza wa Diamond, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, yeye alilipatia namna ya kulivaa na kuwaumbua Tanasha na Shilole ambao liliwatia aibu.



TANASHA

Akiwa na Diamond kwenye tukio hilo la Manara lililofanyika katika Ukumbi wa Hyatt Regency The Kilimanjaro Hotel, Posta jijini Dar, Tanasha alikosa kabisa uhuru kufuatia gauni hilo kumvuka na kuacha matiti yake hadharani.



LINAITWA KATA-KIFUA

Gauni hilo maarufu kwa jina la kata-kifua linaloishia kifuani na kuacha mabega wazi lilimfanya Tanasha kushindwa hata kupiga makofi kwani kitendo cha kunyanyua tu mikono na kuachia makwapa, basi lingemvuka lote hadi kiunoni.

Kufuatia hali hiyo, ilibidi Tanasha kulishikilia gauni hilo muda wote huku akimuomba Mungu kimoyomoyo shughuli hiyo imalizike ili aondoke ukumbini hapo kwani alionekana wazi kutokuwa na furaha.



SHILOLE

Miezi kadhaa iliyopita Shilole naye alikuwa gumzo baada ya gauni kama hilo alilokuwa amevaa kwenye pati ya Wasafi Classic Baby (WCB) kumuacha wazi matiti na kumkosesha raha huku akijuta kuvaa nguo hiyo.

Kwenye mitandao ya kijamii, watu walimsimanga mno Shilole kwa kitendo chake cha kuvaa gauni kama hilo na kuacha wazi maungo yake nyeti akiwa ni mwanamke wa Kiislam.


Lakini kama kawaida ya Shilole, siyo mtu wa kuficha mambo, baada ya kuona watu wamemsimanga vya kutosha hakusita kutoa dukuduku lake kuhusu nguo hiyo ambayo iliwaacha watu midomo wazi kwa kumsema.

Shilole alisema kuwa aliliona gauni hilo kwenye mtandao na kuliagiza kwa lengo la kuivaa akiamini kuwa atapendeza na kutokea kama alivyoiona kwenye picha kama ilivyo kawaida ya watu wengi wakiamini kuwa nguo hizo zitawatoa kama walivyoziona katika mtandao.

Shilole alisema: “Yaani kama nitaagiza tena nguo mtandaoni…walahi labda mimi siyo dada Mwajuma.”



ZARI

Baada ya gauni hilo kuwa gumzo, mashabiki wa Zari waliibuka na picha zilizomuonesha mwanamama huyo akiwa amevaa gauni kama hilo na kuwa huru kufanya lolote bila kumvuka.

Picha hizo zilimuonesha Zari akiwa amelivaa gauni kama hilohilo miezi kadhaa iliyopita na kumpendeza bila kujali ni mama wa watoto watano tofauti na Shilole ambaye ni mama wa watoto wawili huku Tanasha akiwa hana mtoto.



MAMA D AMKINGIA KIFUA TANASHA

Wakati mjadala huo ukiwa umenoga huku Tanasha akisemwa kila kona juu ya gauni hilo ndipo alipoibuka ‘mama mkwe’ wake, Sanura Kassim ‘Bi Sandra’ na kumkingia kifua.

Akizungumza na Gazeti la Amani kupitia simu ya kiganjani ya mwanaye Esma Khan, Bi Sandra ambaye ni mama mzazi wa Diamond aliwataka watu wanaomuandama mrembo huyo kuacha kwani wao kama familia wamemkubali alivyo.

“Tanasha ana tabia nzuri na isitoshe ana mapenzi ya dhati kwa familia yetu.



“Anapendwa kushirikiana na familia kwani kuna wakati anaitwa wana familia nyumbani kwake (Mbezi-Beach) na kukaa nao vizuri.

“Kwanza Tanasha hana sifa mbaya na hajawahi kufumaniwa kama wengine,” alisema mama Diamond bila kufafanua aliyefumaniwa ni nani?



ATOA MSIMAMO

Mama huyo aliendelea kufunguka msimamo wa familia kuwa, wanamtambua na kumkubali Tanasha kwani ndiye mwenye vigezo vyote vya kuwa mke wa Diamond.

Kwa upande wake Esma, alisema Tanasha ni zaidi ya wifi kwake kwani anajielewa. Alisema kuhusu mambo mengine yote yanayosemwa kuhusu yeye hawayajali, zaidi wanaangalia tabia zake njema.

DIAMOND NA TANASHA

Diamond na Tanasha wanatarajiwa kutangaza kufunga ndoa muda wowote baada ya kuahirisha zoezi hilo ambalo awali walitangaza lingekuwa ni Februari 14, mwaka huu.

Daimond Awaonya Mbele ya Makonda Wasanii Wanaotoa Rushwa Wasafi Media Ili Ngoma Zao Zichezwe

Daimond Awaonya Mbele ya Makonda Wasanii Wanaotoa Rushwa Wasafi Media I'll Ngoma Zao Zichezwe

Msanii Diamond Platnumz ambae ni bos wa televiesheni ya wasafi ambae pia ni meneja wa ebo ya WCB amefunguka na kuwaonya wasanii ambao wamekuwa wakitoa pesa kwa ajili ya kutaka kupata nafasi za nyimbo zao kupigwa kati atv yake.

Diamond anasema kuwa kwa uande wake alishasema kabisa kuwa kila anaeleta nyimbo yake katika Tv hiyo basi itapigwa lakini kama kuna mtu anakuwa akitaka kutoa pesa ili aweze kupewa muda mwingi wakati kazi yake sio nzuri kuliko wengine basi huyo hana nafasi katika Tv hiyo.



Akiongea katika mkusanyiko mkubwa wa wasanii uliofanyika jana, baada ya mkuu wa mkoa kukutana na wasanii kuzungumzia changamoto za wasanii wa bongo movie , Diamond anasema kuwa tv yake ni bure kabisa na hakuna haja ya kutoa pesa.

Faiza- Nikipata Ukimwi Nitajitangaza Hadharani

Faiza- Nikipata Ukimwi Nitajitangaza Hadharani

Muigizaji wa Bongo movie na mzazi mwenzake na Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Faiza Ally amefunguka na kuweka wazi kusababisha endapo siku akijigundua kuwa ni muathirika basi hatajificha bali atajitangaza hadharani.

Faiza amefunguka kuwa endapo itatokea bahati mbaya akakwaa ugonjwa wa Ukimwi a.k.a ngoma, kamwe hatajificha au kujiona tofauti, bali atajitangaza hadharani na kuwapa watu moyo kuwa wanaweza kuishi miaka mingi zaidi.


Katika mahojiano yake na Gazeti la Ijumaa, Faiza ambaye ni mama wa watoto wawili alisema anawashangaa wenye tatizo hilo ambao hujificha na hata wengine kuambukiza wengine, lakini kwa upande wake ataweka hadharani ili kuwapa elimu wengine na kuzuia maambukizi mapya.

Kama mimi ningekuwa na Ukimwi, ningejitangaza hadharani bila woga wowote wala aibu na tena nitasaidia watu wengine wajiepushe na maambuzi mapya“.

Wiki iliyopita Faiza alizua gumzo kwenye Mitandao ya kijamii Baada ya kuposti video iliyomuonyesha akiwa anapima ugonjwa wa Ukimwi na kuanika majibu yake yaliyoonyesha hana maambukizi ya gonjwa hilo.

Hivi Ndivyo Zari Alivyowaumbua Tanasha na Shilole

Mchumba wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Tanasha Donna Oketch ameendelea kutengeneza vichwa vya habari Bongo, Amani linaye....